IQNA

Khatibu wa Sala ya Ijumaa Tehran

Kundi la kigaidi la Daesh (ISIS) ni chombo cha Marekani na utawala wa Israel

22:07 - January 05, 2024
Habari ID: 3478153
IQNA-Khatibu wa Sala ya Ijumaa ya Tehran amezungumzia jinai ya kigaidi ya Kerman na kukiri kundi la kigaidi la ISIS au Daesh kuhusika na hujuma hiyo na kusema: ISIS ni chombo cha Marekani na utawala wa Kizayuni.

Ayatullah Seyed Ahmad Khatami, khatibu wa Sala ya Ijumaa mjini Tehran amelaani jinai ya kigaidi siku ya Jumatano katika maziara ya mashahidi wa mji wa Kerman huko kusini mashariki mwa Iran. Aidha ameashiria mauaji ya raia 17,000 wa Iran katika hujuma za kigaidi baada ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran na kusema:  Kundi la kigaidi la Daesh (ISIS) liliundwa na  Marekani na ni chombo cha utawala wa Kizayuni wa Israel.

Ikumbukwe kuwa katika hotuba ya kampeni ya Rais wa zamani wa Marekani Donald Trump mwaka 2016, alimtuhumu mtangulizi wake Barack Obama, kuwa ndiye aliyeanzisha kundi la kigaidi la Daesh.

Ayatullah Khatami amesema kuwa, kundi la kigaidi la Daesh lina hasira kwa sababu liliangamizwa Iraq na Syria kufuatia jitihada za Luteni Jenerali Qassem Soleimani aliyeuawa shahidi, na akasisitiza kwamba damu ya mashahidi wa tukio la kigaidi la Kerman italipizwa kisasi.

Shambulio la kigaidi lililotekelezwa juzi Jumatano huko Kerman limeua shahidi watu wasiopungua 89 na kujeruhi wengine 285. Hujuma hiyo ya kigaidi ilitekelezwa katika kumbukumbu ya  kumuenzi Kamanda wa vita dhidi ya ugaidi Shahidi Luteni Jenerali Qassim Soleimani aliyeuliwa kigaidi katika hujuma ya jeshi katili la  Marekani huko Baghdad Iraq miaka minne iliyopita. Kundi la kigaidi la Daesh limedai kuhusika na hujuma hiyo ya kigaidi nchini Iran.

4192130

captcha