kwa mujibu wa mwandishi wa iqna, mashindano hayo ya kuhifadhi qur’ani tukufu kikamilifu yamewajumuisha waalimu kutoka shule 20 za mji huo mkuu wa kenya.
mmoja kati ya wasimammizi wa mashindano hayo sheikh abdul rahman abdul aziz amenukuliwa akisema waliopata pointi bora zaidi katika kuhifadhi kwa kuzingatia kanuni sahihi za qiraa na tajwid wametunukiwa zawadi.
amesema aliyeshika nafasi ya kwanza amepta zawadi ya dola 800, nafasi ya pili 700 na nafasi ya tatu dola 600.