IQNA

Utawala wa Bahrain waakhirisha tena kesi ya Sheikh Issa Qassim

17:15 - September 16, 2016
Habari ID: 3470565
Mahakama ya utawala wa kiimla Bahrain meakhirisha tena kutolewa hukumu dhidi ya Sheikh Isa Qassim.
Hukumu ya kesi ya mwanazuoni mashuhuri wa Kiislamu na kiongozi wa kimaanawi wa harakati ya kimapinduzi ya Wabahrain ilitarajiwa kutolewa jana Alhamisi lakini sasa imeahirishwa hadi tarehe 26 Septemba mwaka huu.
Utawala wa kiukoo wa Aal Khalifa unamtuhumu Sheikh Isa Qassim kwamba anaeneza chuki za kimadhehebu miongoni mwa watu wa  Bahrain. Mbali na hayo utawala huo ulimvua uraia wa Bahrain Sheikh huyo hapo tarehe 20 mwezi Juni uliopita jambo ambalo liliamsha hasira kubwa ya wanachi wa nchi hiyo na wa mataifa mengine huru duniani. Kufuatia hatua hiyo ya kibaguzi ya utawala wa Bahrain, eneo la ad-Diraz lililoko magharibi mwa mji mkuu wa Bahrain limebadilika na kuwa kituo cha mikusanyiko na malalamiko ya kila siku ya Wabahrain dhidi ya ukamdamizaji na uonevu wa utawala wa nchi hiyo dhidi ya mwanazuoni huyo mashuhuri wa Kishia.
Ni uungaji mkono huo mkubwa wa wananchi kwa kiongozi huyo mashuhuri na matokeo hatari ya kuchukuliwa hatua ya kuhukumiwa kwake mahakamani ndiko kumewatia hofu watawala dhalimu wa nchi hiyo na kuwafanya waakhirishe kuhukumiwa kwake. Inaonekana kuwa kwa kuakhirisha mara kwa mara kuhukumiwa mwanazuoni huyo, watawala wa Bahrain wanapima hisia na uungaji mkono wa wananchi kwa kiongozi huyo wakidhani kuwa uungaji mkono huo utapungua na hivyo kupata fursa nzuri ya kumukumu bila ya kuhatarisha utawala wao wa mabavu nchii humo. Jambo linalosahaulika na utawala wa Bahrain ni kuwa hautaweza kufikia malengo yake maovu kwa kuwapokonya uraia na kuwafunga jela wanazuoni na wanafikra walio na fikra kama za Sheikh Isa Qassim.
Utawala huo una wasiwasi mkubwa kwamba kwa kumuhukumu Sheikh Isa Qassim huenda ukachochea zaidi hisia na uungaji mkono wa wananchi kwa kiongozi huyo wa kidini na hivyo kutoweza kudhibiti hali ya mambo nchini na wanamapinduzi wa nchi hiyo. Ni miezi mitatu sasa tokea eneo la ad-Diraz anakoishi Sheikh Qassim limegeuka na kuwa eneo la makabaliano makali kati ya wananachi wanamapinduzi na utawala dhalimu wa Manama. Licha ya utawala huo kutumia mbinu za ukandamizaji na unyanyasaji dhidi ya wanananchi lakini wanachi  ndio wamekuwa washindi wa mwisho kufikia sasa kwa kubuni njia tofauti za kukabiliana na ukandamizaji wa askari jeshi wa utawala huo.
Bahrain imekuwa ikishuhudia maandamano ya amani ya wananchi dhidi ya utawala wa Aal Khalifa tangu mwezi Februari mwaka 2011. Wananchi wa Bahrain wanataka marekebisho ya kisiasa, uhuru, uadilifu, kukomeshwa vitendo vya ubaguzi na kuingia madarakani serikali iliyochaguliwa kwa njia ya kidemokrasia. Utawala wa Bahrain umewanyima wananchi wa nchi hiyo haki zao zote.
3460943
captcha